Monday, August 12, 2013

Ney wa Mitego:Nikifa sitaki kuundiwa kamati

Akifunguka kupitia account zake za facebook na instragram alisema kuwa kuna baadhi ya wasanii wanasubiri wenzao wafe ili waunde kamati ili waweze kuzitafuna pesa kama ilivyokuwa kwenye msiba wa marehemu Albert Mangwea‘Ngwea’.
Aidha amefunguka kuwa ameamua kuzungumza hivyo baada ya kupokea vitisho kutoka kwa baadhi ya wasanii,baada ya kuwadis kupitia ngoma yake aliyoiachia ya…
 
Msanii wa Hip Hop Bongo,Elibarik Emaniel‘Nay wa Mitego amefunguka kuwa kama akifariki 

dunia hataki aundiwe kamati za ajabu ajabu za wasanii wenzake wa muziki huo kwani wengi wao hutumia kamati hizo kama mitaji kwa kutafuna pesa za rambirambi.
Akifunguka kupitia account zake za facebook na instragram alisema kuwa kuna baadhi ya wasanii wanasubiri wenzao wafe ili waunde kamati ili waweze kuzitafuna pesa kama ilivyokuwa kwenye msiba wa marehemu Albert Mangwea‘Ngwea’.

Aidha amefunguka kuwa ameamua kuzungumza hivyo baada ya kupokea vitisho kutoka kwa baadhi ya wasanii,baada ya kuwadis kupitia ngoma yake aliyoiachia ya Salaam Zao kuwa waliochukua pesa za rambirambi za Ngwea warudishe hata kimya kimya kwani muda wanao.
‘Zipo nyingi zingine za vitisho,nitazipost zote watu wangu mujue leo nimeanza na hiyo…! Ukweli unauma sana siogopi vitisho vyenu…pelekeni hela za marehemu hata kimyakimya bado nafasi mnayo,,,mi nikifa sitaki kamati za kwenye msiba wangu maana watu wanafanya misiba yetu mitaji yao’alisema Nay.

ShareThis